Marekani yagusia uwezekano wa kutumia nguvu za jeshi Mashariki ya Kati - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Saturday, November 20, 2021

Marekani yagusia uwezekano wa kutumia nguvu za jeshi Mashariki ya Kati



Marekani imeonya leo kuwa ina uwezo wa kupeleka kikosi kikubwa katika eneo la Mashariki ya Kati wakati ikikabiliwa na maswali juu ya utayari wake wa kutumia nguvu za kijeshi katika ukanda huo.


Matamshi hayo yametolewa na waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin katika mkutano wa mjini Manama, Bahran. Austin ameongeza njia zote ziko wazi ikiwa diplomasia itashindwa katika kuzuia mipango ya nyuklia ya Iran.


Waziri huyo hata hivyo amelazimika kukanusha madai ya kwamba Marekani imekuwa ikisita kutumia nguvu na kwamba itaendelea kujilinda na kutetea maslahi yake. Iran inatarajia kurejea tena katika meza ya mazungumzo na mataifa yaliyo na nguvu duniani, katika mazungumzo yatakayofanyika Novemba 29.


Mazungumzo hayo yanalengo la kufufua mkataba wa nyuklia wa 2015 na uwezekano wa kuondolewa vikwazo iliyowekewa Iran

No comments:

Post a Comment