ZAINA FOUNDATION YASEMA TANZANIA INAKUWA KWA KASI KATIKA MATUMIZI YA MITANDAO YA KIJAMII - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Sunday, April 24, 2022

ZAINA FOUNDATION YASEMA TANZANIA INAKUWA KWA KASI KATIKA MATUMIZI YA MITANDAO YA KIJAMII




Na Mwandishi wetu Dodoma

Dunia kwa ujumla imekuwa kwenye Vita kubwa ya kupambana dhidi ya uhalifu wa Kimtandao,Tanzania imekuwa miongoni mwa Nchi zinazoendelea kwa kasi kubwa kwenye matumizi ya Mitandao ya Kijamii.

Zaina foundation ni miongoni mwa Taasisi yenye msaada mkubwa inayojihusisha na utoaji wa Mafunzo yanayohusiana na Matumizi ya Internet na Haki za Kidijital kwa watumiaji wa mitandao kwa ujumla.

Vilevile Dhana ya uhuru wa Kidigitali inahusiana na ulinzi wa kidigitali na utambuzi wa haki za kidigitali zilizopo kama vile Haki ya Faragha na Uhuru wa Kujieleza, katika muktadha wa teknolojia ya kidigitali pamoja na intaneti.

Haya yote yameelezwa Aprili 23, kwenye semina iliyojumuisha waandishi wa habari na wanaharakati mbalimbali wa mitandao kwenye ukumbi wa mikutano wa Nashera Jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment