NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI ATEMBELEA OFISI ZA POSTA - ZANZIBAR - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, August 31, 2022

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI ATEMBELEA OFISI ZA POSTA - ZANZIBAR

Afisa wa Shirika la Posta Zanzibar Bw. Khamis Ame Mohamed (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohammed Khamis Abdulla kuhusu huduma mbalimbali za Shirika zinazotolewa katika Ofisi za Posta mjini Zanzibar
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohammed Khamis Abdulla (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Shirika la Posta Tanzania pamoja na watendaji wa Wizara hiyo mara baada ya ziara yake katika ofisi za Shirika la Posta, mjini Zanzibar. Wa tatu kulia ni Meneja Mkaazi (TPC) Zanzibar Bw. Ahmad Mohammed Rashid
Picha na Matukio mbalimbali wakati Meneja Mkaazi (TPC) Zanzibar Bw. Ahmad Mohammed Rashid aliposhiriki ziara ya ukaguzi wa minara 42 ya Mawasiliano itokanayo na mradi wa Rural Telecommunication Border & Special Zone Phase 7 (BSZPH7) iliyifanywa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohammed Khamis Abdulla mjini Zanzibar

📍Zanzibar📍
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohamed Khamis Abdulla kwa mara ya kwanza leo tarehe 30 Agosti, 2022, amefanya ziara yake katika katika Ofisi Kuu za Shirika la Posta Tanzania, mjini Zanzibar.

Lengo la ziara yake ni kujionea namna Shirika la Posta linavyofanya shughuli zake katika kuwahudumia wananchi hususani katika eneo la usafirishaji wa barua, nyaraka, mizigo na vipeto, mjini humo

Aidha, Bw. Mohamed Abdulla ametumia nafasi hiyo kulitaka Shirika la Posta Tanzania kuendelea kuboresha mifumo yake ili kurahisisha utendaji kazi utakaowezesha kuendelea kutoa huduma zenye ubora kwa wananchi

Sambamba na hilo, Naibu Katibu Mkuu amelipongeza Shirika la Posta kwa jitihada zake mbalimbali za kuendelea kuboresha huduma zake ili kuendana na maendeleo ya Teknolojia Pamoja na mahitaji ya wananchi.

Ziara ya Naibu Katibu Mkuu ilienda sambamba na ukaguzi wa minara 42 itokanayo na mradi wa "Rural Telecommunication Border & Special Zone Phase 7 (BSZPH7)" iliyojengwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwa kushirikiana na kampuni ya  Tigo-Zantel.

Ukaguzi huo ulifanywa na Naibu Katibu Bw. Mohamed Khamis Abdulla na Posta imeshiriki kama mdau wa Mawasiliano nchini aliyeshiriki ziara hiyo ni Meneja Mkaazi (TPC) Zanzibar Bw. Ahmad Mohammed Rashid

No comments:

Post a Comment