Na Okuly Julius-Dodoma
Akizungumza leo Septemba 16,2022 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa programu ya maendeleo ya sekta ya maji awamu ya tatu Senyamule amesema kuwa Mkoa wa Dodoma bado una changamoto ya maji kwa baadhi ya maeneo huku maeneo ya vijijini ikiwa na asilimia 65.1 ya maji na mjini ni asilimia 57.
Senyamule amesema kuwa Mkoa wa Dodoma ni fahari ya Watanzania hivyo ili iwe fahari kweli kweli haipaswi kuwa na changamoto ya maji.
"Hatuwezi kuwa fahari ya watanzania wakati kuna baadhi ya maeneo hayana huduma ya maji na ili tuwe fahari nikuombe Mheshimiwa Aweso na najua hili unaliweza weka uzito mkubwa katika awamu hii ya tatu kwa Dodoma hii ambapo kila siku tunapokea wageni wengi ambao wanakuwa wakaazi na wanahitaji maji,"Amesema Senyamule
No comments:
Post a Comment