KAMPUNI YA NDEGE YA BOEING KUKIRI MASHTAKA YA ULAGHAI WA JINAI. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Monday, July 8, 2024

KAMPUNI YA NDEGE YA BOEING KUKIRI MASHTAKA YA ULAGHAI WA JINAI.

 


Kampuni ya Boeing yakubali kukiri shtaka la kula njama ya ulaghai baada ya Marekani kupata kampuni hiyo ilikiuka makubaliano yaliyokusudiwa kuifanyia marekebisho baada ya ajali mbili mbaya za ndege zake 737 Max zilizoua abiria 346 na wafanyakazi.


Wizara ya Sheria ilisema mtengenezaji huyo wa ndege pia alikubali kulipa faini ya $243.6m (£190m).


Hata hivyo, familia za watu waliofariki katika safari za ndege miaka mitano iliyopita wameikosoa faini hiyo wakisema kuwa ni "adhabu kidogo" ambayo ingeruhusu Boeing kuepuka kuwajibika kikamilifu kwa vifo hivyo. 


Makubaliano hayo lazima sasa yaidhinishwe na jaji wa Marekani.


Kwa kukiri kuwa na hatia, Boeing itaepuka kesi ya jinai - jambo ambalo familia za waathiriwa zimekuwa zikishinikiza.


Kampuni hiyo imekuwa katika mgogoro kutokana na rekodi yake ya usalama tangu ajali mbili zinazokaribiana kufanana zilizohusisha ndege za 737 Max mwaka 2018 na 2019. Ilisababisha kusimamishwa kwa ndege hizo duniani kwa zaidi ya mwaka mmoja.


Mnamo 2021, waendesha mashtaka walishtaki Boeing kwa shtaka moja la kula njama za kuwalaghai wasimamizi, wakidai kuwa ilidanganya Utawala wa Usafiri wa Anga (FAA) kuhusu mfumo wake wa kudhibiti ndege, ambao ulihusishwa na ajali zote mbili.


Ilikubali kutoshtaki Boeing ikiwa kampuni hiyo italipa faini na kukamilisha kwa mafanikio kipindi cha miaka mitatu cha kuongezeka kwa ufuatiliaji na utoaji wa taarifa.


Lakini mnamo Januari, muda mfupi kabla ya muda huo kukamilika, mlango wa ndege ya Boeing inayoendeshwa na Shirika la Ndege la Alaska ulifunguka mara baada ya kupaa na kuilazimisha ndege hiyo kutua.


Hakuna aliyejeruhiwa wakati wa kisa hicho lakini ilizidisha uchunguzi juu ya maendeleo kiasi gani Boeing ilikuwa imefanya katika kuboresha rekodi yake ya usalama na ubora.


Mnamo mwezi Mei, Wizara ya Sheria ilisema imepata Boeing ilikiuka masharti ya makubaliano, na kuongeza uwezekano wa kampuni hiyo kufunguliwa mashtaka.

No comments:

Post a Comment