
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa Mei 29, 2025 alikutana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge wa Japan cha Urafiki na Afrika (Africa Union Parliamentarians Friendship) Mheshimiwa Ichiro Aisawa, kwenye Ofisi za Bunge la Japan.
Katika mazungumzo yao walijadili kuhusu kuendeleza urafiki kati ya Bunge la Tanzania na Bunge la Japan.
Pia, walijadili kuhusu masuala mbalimbali ya uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Japan, pamoja na kumkaribisha kutembelea Tanzania ili kujionea vivutio mbalimbali ya utalii.



No comments:
Post a Comment