OR - TAMISEMI
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia afya Mhe. Dkt. Festo Dugange amewalekeza Wakurugenzi wa Halmashauri kufanya msawazo wa watumishi wa sekta ya afya ili kukizi mahitaji ya wananchi wakati ambapo Serikali inaendelea kutoa vibali vya ajira katika sekta hiyo.
Dkt. Dugange amesema hayo tarehe 9 Juni, 2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Jimbo la Bukene aliyeuliza
Je, lini Serikali itamaliza tatizo la upungufu wa watumishi wa kada ya Afya - Bukene.
“Katika maeneo yote ya zahanati yenye mtumishi mmoja fanyeni msawazo sahihi wa ndani wa watumishi kutoka kwenye vituo vyenye watumishi wengi ili kuendelea kutoa huduma muhimu kwa wananchi” Mhe. Dkt. Dugange
Serikali inaendelea kutoa vibali vya ajira kila mwaka, ambapo kuanzia mwaka wa fedha 2020/21 hadi 2024/25 jumla ya watumishi wa kada ya afya 34,720 wameajiriwa na kupangiwa vituo.
Amesema katika kipindi cha mwaka 2020/21 hadi 2024/25 halmashauri ya Wilaya ya Nzega imepangiwa jumla ya watumishi 111 ambao wamepangwa katika hospitali ya wilaya, vituo vya afya na zahanati. Kati ya hao, jimbo la Bukene limepelekewa jumla ya watumishi 59.
Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa sekta ya afya kwa awamu na kuwapanga katika maeneo yenye upungufu wa wataalamu hao ikiwemo halmashauri ya wilaya ya Nzega.
No comments:
Post a Comment