WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa leo Juni 24, 2025 amezindua mitambo ya uchorongaji na vifaa vya utafiti kwa wachimbaji wadogo kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) katika hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Utoaji wa mitambo hiyo ni utekelezaji wa maono na msukumo wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwawezesha wachimbaji wadogo kutokana na mchango wao katika kuzalisha ajira, kuboresha kipato cha mtu mmoja mmoja na kukuza uchumi wa Taifa.
No comments:
Post a Comment