TFRA Yawahakikishia Wakulima Upatikanaji wa Mbolea kwa Wakati - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, August 5, 2025

TFRA Yawahakikishia Wakulima Upatikanaji wa Mbolea kwa Wakati

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent, akipokea kifungashio kutoka kwa Justine Nassari wa kiwanda kinachozalisha mbolea za kimiminika cha Keen Feeders LTD cha Arusha Nchini Tanzania kama ukumbusho wa kutembelea banda hilo wakati wa maonesho ya wakulima nanenane katika viwanja vya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma tarehe 5 Agosti, 2025.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent akifafanua jambo kwa mkulima aliyetembelea banda la Mamlaka ndani ya hema la Kijiji cha mbolea lililopo ndani ya viwanja vya Nanenane vya Nzuguni Jijini Dodoma tarehe 5 Agosti, 2025
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent (kushoto) akipokea maelezo ya namna walivyojipanga kusambaza mbolea kwa wakulima msimu wa Kilimo 2025/2026 kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Kilimo wa kiwanda cha Mbolea cha Minjingu, Dkt. Mshindo Msola alipotembelea kijiji cha mbolea katika viwanja vya nanenane Nzuguni Jijini Dodoma tarehe 5 Agosti, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Bw. Joel Laurent, amewahakikishia wakulima upatikanaji wa mbolea kwa wakati kwa kuzingatia mahitaji ya msimu wa kilimo kwa mwaka 2025/2026.

Joel ametoa kauli hiyo leo alipofanya ziara katika Kijiji cha Mbolea kilichopo kwenye viwanja vya Maonesho ya Nanenane, Nzuguni mkoani Dodoma.

Amesema kuwa ili kuhakikisha mbolea zinafika kwa wakulima kwa urahisi, serikali inapanga bei za pembejeo hizo kwa kuzingatia umbali mkulima aliko na hivyo kuwapa motisha wasambazaji na mawakala wa mbolea kufikisha pembejeo hiyo maeneo ya pembezoni. 

“Tunaendelea kuhakikisha kwamba mbolea zinapatikana kwa wakati na kwa bei himilivu inayozingatia umbali kutoka katika chanzo,” ameongeza Joel.

Katika kuimarisha uwekezaji wa viwanda vinavyozalisha mbolea nchini, Joel amesema, katika msimu wa kilimo wa 2025/26 serikali imepanga kufanikisha ununuzi na upatikanaji wa kiasi cha tani 200,000 za mbolea kutoka kwa wazalishaji wa ndani pamoja na tani 50,000 za Chokaa mazao na kuzisambaza kwa wakulima nchini

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Kilimo wa Kiwanda cha Mbolea cha Minjingu, Dkt. Mshindo Msolla, amesema kuwa kampuni hiyo imejipanga kuongeza uzalishaji wa mbolea zinazozingatia mahitaji halisi ya udongo kwa kila eneo nchini, kufuatia matokeo ya tafiti walizozifanya wakati wa majaribio ya mbolea zao.

No comments:

Post a Comment