AFDP YADHAMIRIA KUONGEZA UPATIKANAJI WA MBEGU BORA NCHINI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Sunday, September 7, 2025

AFDP YADHAMIRIA KUONGEZA UPATIKANAJI WA MBEGU BORA NCHINI



Kilosa, Morogoro


Ujumbe wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kwa kushirikiana na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), umesema utaendelea kuwekeza katika uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora ili kuongeza tija kwa wakulima nchini.

Kauli hiyo imetolewa na kiongozi wa ujumbe huo, Bi. Nester Mashingaidze, alipozungumza na wakulima wa Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro, alipokuwa akikagua utekelezaji wa programu hiyo inayolenga kuongeza uzalishaji wa mahindi, alizeti, maharage na mimea jamii ya mikunde.

“Tunalenga kuongeza upatikanaji wa mbegu bora kwa kushirikiana na taasisi kama TARI, ASA, na TOSCI ili kuwafikia wakulima wengi zaidi kwa wakati,” alisema Bi. Mashingaidze.

Kwa upande wake, Bw. Salum Mwinjaka – Mratibu wa Programu hiyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema AFDP inatekelezwa katika mikoa 11 ya Tanzania Bara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba. Alibainisha kuwa programu inajikita katika kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi, lishe na usawa wa kijinsia.

Naye, Mhandisi Enock Nyanda kutoka TAMISEMI, alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wizara za kisekta kufikisha huduma kwa wananchi kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo.

Wakulima waliopokea mafunzo kutoka kwenye programu hiyo wamesema imewasaidia kuachana na kilimo cha mazoea na kuhamia kwenye kilimo chenye tija kwa kutumia mbegu bora na za kisasa.

No comments:

Post a Comment