Maelfu ya wananchi na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM wakiwa wameujaza uwanja wa Azimio Wilayani Mpanda Mkoani Katavi leo Jumamosi Oktoba 18, 2025 ili kumlaki na kumsikiliza Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan anayeanza Kampeni zake hii leo kwenye Mkoa huo wa Katavi pamoja na Mkoani Rukwa. Uchaguzi Mkuu unafanyika Oktoba 29, 2025, na Dkt. Samia anatumia mikutano hiyo kunadi ilani ya Chama chake, kueleza mafanikio ya serikali yake ya awamu ya sita na kuwaomba kura Watanzania.
Saturday, October 18, 2025
New
MPANDA WAUJAZA UWANJA WA AZIMIO, KAMPENI ZA DKT. SAMIA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment