
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akizungumza wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.
.......
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amesema Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeleta mageuzi makubwa katika Biashara ya mazao nchini katika kipindi cha miaka mitano (2019–2025), hatua iliyoongeza tija kwa wakulima na mapato ya Serikali.
Mhe. Kapinga ameyasema hayo Disemba 12, 2025 jijini Dodoma wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB alipobainisha kuwa mageuzi hayo yameongeza ufanisi, uwazi na matumizi ya TEHAMA katika minyororo ya biashara ya mazao nchini.
Aidha, kiasi cha mazao yanayopitia mfumo huo kimeongezeka kwa zaidi ya asilimia 120, kutoka chini ya tani 600,000 hadi zaidi ya tani 1.3 milioni kwa mwaka, huku bei za mazao zikiongezeka kwa wastani wa asilimia 15 hadi 35, na hivyo kuongeza kipato cha maelfu ya wakulima.
Pia amesema kuwa idadi ya maghala yaliyosajiliwa imeongezeka kutoka chini ya 300 hadi zaidi ya 500, huku mapato ya Serikali yakipanda kwa zaidi ya asilimia 140 kutokana na ushuru, kodi na tozo mbalimbali.
Waziri Kapinga ameielekeza Bodi mpya kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaimarishwa na kupanuliwa zaidi katika kipindi kijacho cha miaka mitano huku akiitaka bodi hiyo Mpya kuongeza ufanisi, uwajibikaji na ushindani katika biashara ya mazao nchini.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, amesema kuwa wizara hiyo itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Kilimo ili kuboresha huduma za masoko na kuongeza tija kwa wakulima nchini pamoja na kuimarisha uwezo wa wakulima, kukuza ajira na kuunganisha kilimo na viwanda ili kuchochea maendeleo endelevu ya taifa.
Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu, amebainisha kuwa matumizi ya stakabadhi yameendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka, ambapo idadi ya stakabadhi imepanda kutoka 33,100 hadi 53,107 kwa mwaka 2024/2025, hatua inayoonyesha kuongezeka kwa uelewa na mwitikio wa wakulima na wafanyabiashara.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu,wakati alipowasili kwa ajili ya kuzindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akizungumza wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Naibu Waziri Wa Kilimo Mh.David Silinde ,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, wakati wa uzinduzi wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (hayupo pichani) wakati akizindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua Bodi mpya ya Wakurugenzi wa WRRB) hafla iliyofanyika leo Disemba 12,2025 jijini Dodoma.

No comments:
Post a Comment