DKT. MSONDE AWATAKA NCC KUWA WABUNIFU - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, April 28, 2026

DKT. MSONDE AWATAKA NCC KUWA WABUNIFU


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Dkt. Charles Msonde amezungumzia umuhimu wa Watumishi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), kuwa wabunifu, wenye umoja na mshikamano ili kuliwezesha Baraza hilo kufanya kazi na kuleta tija kwa Taifa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi jijini Dodoma leo Dkt. Msonde, amesema kila mtumishi wa NCC ajue anajukumu la kujadili mipango ya maendeleo na kubuni ufumbuzi utakaoleta manufaa kwa Taifa.

"Tambueni NCC ina dhima kubwa kwenye tasnia ya ujenzi nchini hivyo msiogope changamoto kwani hizo ndizo huleta mchakato wa maendeleo", amesisitiza Dkt. Msonde.

Amesisitiza kuwa katika utumishi wa umma mafanikio makubwa yanapatikana pale watumishi wanaposhirikiana, kusaidiana na kufanya kazi kwa weledi na bidii.

“Katika utumishi wenu wa NCC muwe na uwezo wa kushiriki katika kupanga mipango ya maendeleo yenye tija katika Taasisi yenu, mjitahidi kubuni mambo mapya kuepuka migogoro na kujiepusha na mgongano wa maslahi”, amesisitiza Dkt. Msonde.

Dkt. Msonde amesema Wizara itakuwa pamoja na NCC katika kuwezesha mipango yote itakayopangwa kuhakikisha Taasisi hiyo inakuwa na kuboresha Tasnia ya Ujenzi nchini.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa NCC ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Dkt. Matiko Mturi amesema NCC imeendelea kuratibu usuluhishi wa migogoro inayotokea katika miradi ya ujenzi pamoja na kupata mashauri mapya ambayo yanafanyiwa kazi na kukuza tasnia ya ujenzi nchini.

Aidha, Dkt. Mturi amesema Baraza la Taifa la Ujenzi limeweza kutoa mafunzo kwa wadau wa Sekta ya Ujenzi hususani katika maeneo ya kusimamia mabadiliko ya mikataba.




No comments:

Post a Comment