Na Mwandishi wetu - Dodoma.
Mashindano ya Bahi Kijani Cup 2026 yanatarajiwa kuanza rasmi jumapili septemba 6, 2026, kwa mchezo wa ufunguzi utakaowakutanisha magwiji wa soka Bahi na Ilindi kwenye Uwanja wa Bahi sokoni kuanzia saa 10 jioni.
Kabla ya kuanza kwa mchezo huo kutafuatia na sherehe za uzinduzi (Burudani) ambapo wasananii mbalimbali watasherehesha.
Mashindano hayo yanayotajwa kuwa na ushindani wa hali ya juu kwani yameanzishwa kwa lengo la kuibua na kukuza vipaji vya soka kwa vijana,kutoa fursa ya viongozi kukutana na vijana na kusikiliza changamoto zao na kisha kuziwasilisha kwenye mamlaka husika kwaajili ya utatuzi ,halikazarika kuimarisha mshikamano wa jamii pamoja na kuhamasisha maendeleo ya michezo katika wilaya ya Bahi .
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dodoma, mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa vijana wa CCM wilaya ya Bahi Justine Lucas Sangulah amesema maandalizi yote ya ligi hiyo yamekamilika kinacho subiriwa ni kuanza kwa mtanange wa kumpata mshindi huku akibainisha mpaka sasa timu 24 kutoka kata 22 za Bahi zenye jumla ya vijiji 59 na vitongoji zaidi ya 500 zimejisajili kuwa tayari kwa mwandindano.
Bahi kijani Cup 2026 itazikutanisha timu mbalimbali kutoka kata tofauti za jimbo hilo, huku zikitarajiwa kuonyesha ushindani mkubwa katika kuwania ubingwa wa mashindano hayo kutokana na zawadi Nono zilizowekwa na waandaaji kwa mshindi wa kwanza, wapili na watatu .
“mauli mbiu ya Bahi Kijani Cup ni VIJANA
NA FURSA, TUNAONGEZA TABASAMU” na hii imedhihirika kwa vitendo kwani zawadi zilizoandaliwa kwa washindi ni kama ifuatavyo,mshindi wa kwanza atapewa pair ya ngombe wa maksai (ng’ombe wawili wa kulima)
jembe la kuvutwa na ng’ombe na joki lake kwa maana hawa washindi tayari tutawasaidia kutengeneza kikundi na tayari wataenda kulima na kufanya shughuli zingine za kijamii, kadhali mshindi wa pili tutampatia mbuzi wawili na mshindi wa tatumbuzi mmoja, hivyo itoshe tu kusema hii sioya kukosa",. amesema.
aidha Sangulah amebainisha wadau watakao hudhuria katika hafra ya uzinduzi huo akiwataja Ofisi ya Maendeleo ya jamii Kutoka Halmashauri huku akimtaja Mgeni rasmi atake Fungua mashindano hayo ambae ni MNEC na Katibu wa UVCCM Taifa Halid Mwinyi .
amesema Baada ya mchezo wa ufunguzi, ratiba ya michezo mingine itaendelea kama ilivyopangwa na waandaaji, huku timu zikitarajiwa kuendelea kushindana katika hatua za awali.
Wananchi wa Bahi na maeneo ya jirani wamealikwa kujitokeza kwa wingi kushuhudia michezo hiyo na kuwa sehemu ya mafanikio ya Bahi kijani Cup 2026.


No comments:
Post a Comment