Waziri
 Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametoa ufafanuzi kuhusu mjadala 
ulioibuka kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutoonekana kwenye misiba 
ya aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta na waziri wa Elimu wa zamani, 
Joseph Mungai.
Sitta
 alifariki Novemba 7 mwaka huu nchini Ujerumani alipokuwa ameenda 
kutibiwa maradhi ya tezi dume ambapo siku iliyofuata alifariki Mungai.
Lowassa amesema kuwa hakuweza kuhudhuria kwakuwa alikuwa nchini Afrika Kusini akimuuguza mdogo wake, Bahati Lowassa.
“Mdogo
 wangu Bahati Lowassa ni ofisa ubalozi nchini Afrika Kusini, alikuwa 
anaumwa na alikuwa amelazwa. Kwa siku zote nilikuwa huko kumuangalia. 
Nisingeacha kuhudhuria misiba hiyo,” Lowassa 
Mwanasiasa
 huyo ameongeza kuwa alikuwa pamoja na waombolezaji kwa kutuma salamu 
zake za rambirambi kwa familia ya Sitta kupitia vyombo vya habari pamoja
 na kumtumia mwanasheria wake kuwasilisha salamu zake za rambirambi kwa 
familia ya Mungai.


No comments:
Post a Comment