
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameliagiza jeshi la Magereza na idara zingine zenye mashirika ya uzalishaji ambazo zipo chini ya wizara yake zifanye uzalishaji mali pamoja na kuwatumia wafungwa katika kufanya kazi ndani ya jeshi.
Waziri
 Nchemba ameongea hayo akiwa katika ufunguzi wa nyumba tano za maaskari 
wa jeshi la magereza mkoa wa Arusha nyumba zilizojengwa kwa kutumia 
fedha za shirika la magereza la uzalishaji mkoani humo.
Mh.
 Nchemba ametoa rai kwa jeshi hilo kuona kama inawezekana jeshi hilo 
kutumia wafungwa ambao wamemaliza mafunzo yao na wakaona wamerekebika 
kitabia na kuwachukua waendelee kufanya kazi kwa mkataba katika 
mashirika hayo kwani itarahisisha kupunguza wahalifu zaidi kuliko kwenda
 uraiani wakiwa hawana uwezo wakufungua biashara na kurudia makosa.
Naye
 mkuu wa Magereza Tanzania Dr Juma Malewa amewataka wananchi na 
mashirika ya umma na serikali kutumia jeshi la Magereza nchini katika 
shughuli za ujenzi kwani gharama zake ni nafuu sana lakini zenye ubora 
zaidi.
Kwa
 upande wa Mkuu wa Jeshi la Magereza mkoa wa Arusha, Hamis Nkabasi 
amesema nyumba hizo zimetumia gharama ndogo za ujenzi kwasababu 
rasilimali watu wametumia askari wenye ujuzi wa ujenzi na wafungwa 
ambapo imegharimu milioni 50 kila nyumba na itaweza kuchukua askari 12 
ambapo zote zitachukua askari 60 na kama wangechukua kampuni kujenga 
basi ingegharimu fedha nyingi zaidi.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment