Afisa
huduma na mtoa elimu kwa mlipa kodi mkoa wa Dodoma Barnabas Masika amewataka
wananchi wa mkoa wa Dodoma wanapo nunua chombo cha moto wafike ofisi za TRA
kabla ya mwezi mmoja [siku 30] kuisha ili kubadili umiliki.
Ameyasema hayo wakati wa hitimisho ya mafunzo ya elimu ya usalama barabarani kwa
waendesha pikipiki yaliyo fanyika katika kata ya Haneti Wilayani chamwino mkoani dododma na kuwataka wananchi wazingatie elimu wanayo
pewa na wakufunzi wao wakiongozwa
na FAUSTIN MATINA ili kuondokana na
tatizo la ajali barabarani .
Pia amewaasa madereva bodaboda waliopata mafunzo na
kutunukiwa vyeti wafanye utaratibu wa
malipo ili waweze kupata leseni halisi ya udereva kwa haraka.
Aidha kwa
upande wake mkuu wa kituo cha polisi cha haneti [OCS] MOHAMED JUMA ALLY amewaasa madereva bodaboda walio tunukiwa
vyeti kupata leseni zao ili kuondoka na usumbufu barabarani na amewataka bodaboda wengine kuiga mfano kwa
wale waliopata mafunzo na kutunukiwa
vyeti na pia kuwataka wale wote ambao
hakupata mafunzo wajiunge na mafunzo hayo ili kupunguza ajali barabarani na kusema kuwa wale wasiotaka kupata elimu
hiyo ni sawa na waahalifu maana lengo la elimu hiyo ni kuwa na uelewa
wakati wa unaendesha pikipiki.
“lengo letu sisi polisi pamoja na wakufunzi
wanaoongozwa na Faustin Matina ni kupunguza ajali za kizembe na wala sio
vinginevyo na kwa wale ambao hawakushiriki mafunzo haya ni sawa na waalifu
wengine tu kwa sababu sifa kubwa ya mwalifu ni kukwepa vitu vizuri na vya
kimaendeleo kwa lengo la kuendelea na uhalifu wao hivyo nitapambana nao’’ Alisema Mohamedi Ally
Pamoja na
hayo Mkuu huyo wa kituo cha polisi amewataka bodaboda wote kuhakikisha kuwa wanakata leseni ndani ya
muda stahiki ili kuepukana na usumbufu wawapo katika shughuli zao za kila siku.
Pia ametoa ushauri kwa wakufunzi kuwa elimu hii
isiwe mwisho katika kata yake bali iwe endelevu na mwakani waje tena ila katika
kipindi ambacho wakulima ndio wanatoka kuvuna kwa sababu kipindi hiki sio
kizuri kwa sababu wengi wao ndio wanatayarisha mashamba kwa ajili ya kilimo
hivyo wanakosa pesa kwa ajili ya kushiriki mafunzo na kupata kila kitu
kinachohitajika kwa wakati.
Elimu
hiyo inayotolewa na chuo cha WIDE INSTITUTE OF DRIVING chenye makao
makuu yake mkoani Kilimanjaro inaendelea katika wilaya za Kondoa na
Chemba mkoani Dodoma.
HABARI PICHA
HABARI PICHA
![]() |
Mkuu wa kituo cha polisi HANETI akizungumza na washiriki wa mafunzo (Picha na Okuly julius) |
![]() |
Afisa
huduma na mtoa elimu kwa mlipa kodi mkoa wa Dodoma Barnabas Masika akitoa elimu kwa washiriki wa mafunzo ya usalama barabarani kata ya HANETI wilayani CHAMWINO (Picha na Okuly Julius) |
![]() |
Washiriki wakiwa makini kusikiliza Elimu inayotolewa |
![]() |
Msoma risala akiwasilisha mawazo na mapendekezo ya wenzake mbele ya mgeni rasmi. |
![]() |
Wahitimu wa mafunzo hayo baada ya kukabidhiwa vyeti vyao katika picha ya pamoja na wageni rasmi na watoa elimu hiyo baada ya mafunzo kufungwa.(Picha na Okuly Julius) |


No comments:
Post a Comment