WATU 6 WA FAMILIA MOJA WAPOFUKA GHAFLA KATIKA MAZINGIRA TATANISHI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Monday, November 29, 2021

WATU 6 WA FAMILIA MOJA WAPOFUKA GHAFLA KATIKA MAZINGIRA TATANISHI



Wakazi wa kijiji cha Thim Jope, Uriri, kaunti ya Migori nchini Kenya wamepigwa na bumbuwazi baada ya watu wa familia moja kupofuka katika hali tatanishi.


Katika kisa kisichokuwa cha kawaida, Hellen Achieng' na wanawe wanne wenye umri wa kati ya miaka saba na 24 walipofuka ghafla kabla ya kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Migori kwa matibabu.


George Omondi aliambia Nation kuwa mpwa wake mwenye umri wa miaka 12, ambaye alikuwa anaishi na familia hiyo, alianza kutetemeka baada ya kupoteza uwezo wa kuona na kisha baadaye alizirai na kufariki dunia.


No comments:

Post a Comment