Rais Samia akutana na Mbowe Ikulu - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Saturday, March 5, 2022

Rais Samia akutana na Mbowe Ikulu


Rais Samia Suluhu Hassan  akizungumza  na Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe


Dar es salaam 

RAIS Samia Suluhu Hassan leo amekutana na Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo.

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Zuhura Yunus imesema kuwa Mwenyekiti huyo amemshukuru Rais Samia kwa kuonesha kujali kwake  huku akikubali kwa msingi mkubwa wa kujenga Taifa la Tanzania ni kusimamia haki.

Pia Mbowe ameeleza kwamba wamekubaliana kufanya siasa za kistaarabu  na za kiungwana na kwamba yupo tayari kushirikiana na serikali katika kuleta maendeleo ili nao waweze kutekeleza  majulumu yao ipasavyo.

" Rais Samia amesisitiza kuwa kuna umuhimu wa kushirikiana ili kuijenga Tanzania kwa kuaminiana na kuheshimiana kwa misingi ya haki," ilisema taarifa hiyo.

Mbowe na wenzake watatu wameachiliwa huru baada ya mwendesha Mashtaka mkuu wa serikali kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi katika Mahakama ya Divisheni ya makosa ya rushwa na uhujumu uchumi.

Mahakama hiyo ilikuwa ikiwashikilia kwa kesi ya kujibu kuhusu tuhuma mbalimbali zikiwamo za kupanga njama za kufanya vitendo vya kigaidi.

Kesi hiyo ilikuwa ikisimamiwa na jaji Joachim Tiganga.


No comments:

Post a Comment