KUTOKA JELA HADI KUWA RAISI MWENYE UMRI MDOGO KUCHAGULIWA AFRIKA. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Thursday, March 28, 2024

KUTOKA JELA HADI KUWA RAISI MWENYE UMRI MDOGO KUCHAGULIWA AFRIKA.

"Sikuwahi kuzingatia kujiingiza katika siasa kamwe ," anasema mtoza ushuru huyo wa zamani na mume kwa wake wawili.”

Wachache walikuwa wamesikia kumhusu mwaka mmoja uliopita, na sasa anatazamiwa kuwa rais.


Kuinuka kwa njia ya ajabu kwa Bassirou Diomaye Faye kunafikia kipindi cha hali ya juu katika siasa za Senegal ambazo ziliwavutia watu wengi.


Miezi ya kukaa jela pamoja na mshirika na mwanasiasa mwenye ushawishi Ousmane Sonko iliisha ghafla, wawili hao wakiachiliwa wiki moja kabla ya uchaguzi wa urais.



Sasa 'Bw Safi', kama anavyoitwa kwa jina la utani, lazima aanze kufanyia kazi mageuzi makubwa aliyoahidi.





"Anayependa utaratibu" na "Asiye wa kujionyesha" ni maneno yanayotumiwa mara nyingi kuelezea mtoza ushuru huyo wa zamani ambaye alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ya mwaka 44 ,Jumatatu.


Bw Faye anakumbuka kwa furaha maisha yake ya kijijini huko Ndiaganiao, ambapo anasema yeye hurudi kila Jumapili kufanya kazi ya shamba.


Upendo na heshima yake kwa maisha ya kijijini inalingana na kutokuwa na imani kubwa na wasomi wa Senegal na walio katika siasa za sasa.


"Hajawahi kuwa waziri na hakuwa kiongozi wa serikali hivyo wakosoaji wanahoji ukosefu wake wa uzoefu," 


"Lakini, kwa mtazamo wa Faye, watu wa ndani ambao wameendesha nchi tangu 1960 wameshindwa kwa kiasi kikubwa."


Kupambana na umaskini, ukosefu wa haki na ufisadi ni ajenda kuu ya Bw Faye. Walipokuwa wakifanya kazi katika Hazina ya kitaifa , yeye na Bw Sonko waliunda jopokazi la muungano ili kukabiliana na ufisadi.


Makubaliano ya gesi, mafuta, uvuvi na ulinzi lazima yote yajadiliwe upya ili kuwahudumia vyema watu wa Senegal, anasema Bw Faye.




Anaanzisha enzi ya "uhuru" na "mpasuka" kinyume na zaidi ya hayo, aliwaambia wapiga kura, na hiyo ni kweli hasa kwa uhusiano na Ufaransa.


Rais mteule wa Senegal anasema kuwa ataondoa sarafu ya CFA franc ambayo inakosolewa sana, ambayo imeegemezwa kwenye euro na kuungwa mkono na mkoloni wa zamani Ufaransa.


Bw Faye anataka kubadilisha sarafu mpya ya Senegal, au eneo la Afrika Magharibi, ingawa hii haitakuwa rahisi.


"Itabidi ashughulikie uhalisia wa bajeti kwa kuanzia... Lakini naona kwamba ana matamanio mengi," Waziri Mkuu wa zamani Aminata Touré, ambaye alihudumu chini ya Rais anayeondoka Macky Sall, anaiambia BBC.


Kuimarisha uhuru wa mahakama na kuunda nafasi za kazi kwa vijana wengi wa Senegal pia ni vipaumbele muhimu kwa Bw Faye - ambayo "Rais Sall aliyapuuza sana na yakamrudi", Bi Touré anaongeza.




Yeye sio kigogo pekee wa kisiasa ambaye amemuunga mkono Faye mwenye umri wa miaka 44 - Rais wa zamani Abdoulaye Wade alifanya vivyo hivyo siku mbili tu kabla ya kura ya Jumapili.


Ni mabadiliko ya ajabu kwa Bw Faye ambaye alikaa gerezani miezi 11 iliyopita kwa mashtaka ya uasi, na miaka mingi zaidi kabla ya hapo chini ya kivuli cha mshirika wake.

No comments:

Post a Comment