Katika zoezi hilo DUWASA imebaini kuzidiwa na miundombinu ya majitaka eneo la Makole kutokana na baadhi ya wananchi kutokuzingatia matumizi sahihi ya miundombinu hiyo kwa kutupa taka ngumu katika chemba za majitaka na hivyo kusababisha kuziba kwa miundombinu ya majitaka.
Meneja wa Majitaka na Usafi wa Mazingira DUWASA, Mhandisi Daniel Mgunda amesema zoezi hilo ni endelevu ili kuhakikisha mazingira yanakuwa safi.
Naye Rahel Muhando, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma DUWASA, amewataka wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya miundombinu ya majitaka kwa usalama wa afya.
#usafiwamazingiraniutu
No comments:
Post a Comment