
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametembelea mradi wa nishati safi ya kupikia wa shule ya Sekondari ya Wasichana Simiyu iliyopo Bariadi mkoani humo na kupewa maelezo na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga wakati akifungua shule hiyo leo tarehe 16 Juni, 2025
Mradi huo unahusisha usimikaji wa mfumo wa kupikia kwa kutumia gesi yaani LPG, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa, hivyo kuchangia katika utunzaji wa mazingira na kulinda afya ya wanafunzi na walimu.
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa ufadhili wa kiasi cha Shilingi Shilingi Milioni 14 kwa ajili ya ujenzi na usimikaji wa miundombinu ya nishati safi ya kupikia katika shule hiyo.








No comments:
Post a Comment