Zanzibar Yachota Uzoefu Dodoma: Yajiandaa Kujenga Mji wa Serikali Kisakasaka - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, August 12, 2025

Zanzibar Yachota Uzoefu Dodoma: Yajiandaa Kujenga Mji wa Serikali Kisakasaka


Kamati ya wataalamu kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Ikiingozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Dkt. Islam Seif Salum imetembelea miradi mikubwa jijini Dodoma ikiwemo Mji wa Serikali Mtumba na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, kujifunza utekelezaji wa Ujenzi wa Mji wa Serikali.

Ziara hiyo inalenga kuandaa mazingira ya ujenzi wa ofisi za Serikali na Baraza la Wawakilishi eneo la Kisakasaka, Zanzibar.

Viongozi hao wamempongeza Rais Dkt. Samia kwa kuimarisha maendeleo ya Makao Makuu ya Nchi kupitia miradi ya kimkakati.




No comments:

Post a Comment