WAGONJWA WENYE MAWE KWENYE MFUMO WA MKOJO WAKITOLEWA MAWE KWENYE FIGO SASA KUKAA WODINI MASAA 24 BADALA YA SIKU 5 - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Thursday, October 23, 2025

WAGONJWA WENYE MAWE KWENYE MFUMO WA MKOJO WAKITOLEWA MAWE KWENYE FIGO SASA KUKAA WODINI MASAA 24 BADALA YA SIKU 5



Na. Jeremiah Mbwambo
Dodoma


Hayo yamesemwa na Daktari Bingwa wa mfumo wa mkojo Okoa Sukunala wakati wakiendelea na matibabu ya kuondoa mawe kwenye mfumo wa mkojo katika kambi maalumu inayo endeshwa na madaktari bingwa wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa Hospitali ya ACIBADEM ya nchini Uturuki

"Hospitali ya Benjamin Mkapa inavifaa vya kisasa vinavyo wezesha kufanya matibabu ya kutoa mawe kwenye mfumo wa mkojo bila kufungua mwili ni kwakutumia matundu madogo (laparoscopic)" amesema Dkt. Okoa

Ameongeza kuwa kunafaida nyingi za kutumia teknolojia hii ya matibabu

"faida ni nyingi lakini nieleze moja kubwa ambayo inamuondolea adha mgonjwa akishafanyiwa matibabu haya atakaa wodini kwa muda usiozidi masaa 24, ambapo awali ilikuwa inamlazimu kukaa wodini siku tano" amesema Dkt. Okoa

Hospitali ya Benjamin Mkapa inaadhimisha miaka kumi ya utoaji huduma huku ikiendelea kuboresha huduma zake huku ikijikita katika matibabu ya teknolojia ya hali ya juu





No comments:

Post a Comment