
Na. Jeremiah Mbwambo
Dodoma
Hayo yamesemwa na Daktari Bingwa wa mfumo wa mkojo Okoa Sukunala wakati wakiendelea na matibabu ya kuondoa mawe kwenye mfumo wa mkojo katika kambi maalumu inayo endeshwa na madaktari bingwa wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa Hospitali ya ACIBADEM ya nchini Uturuki
"Hospitali ya Benjamin Mkapa inavifaa vya kisasa vinavyo wezesha kufanya matibabu ya kutoa mawe kwenye mfumo wa mkojo bila kufungua mwili ni kwakutumia matundu madogo (laparoscopic)" amesema Dkt. Okoa
Ameongeza kuwa kunafaida nyingi za kutumia teknolojia hii ya matibabu
"faida ni nyingi lakini nieleze moja kubwa ambayo inamuondolea adha mgonjwa akishafanyiwa matibabu haya atakaa wodini kwa muda usiozidi masaa 24, ambapo awali ilikuwa inamlazimu kukaa wodini siku tano" amesema Dkt. Okoa
Hospitali ya Benjamin Mkapa inaadhimisha miaka kumi ya utoaji huduma huku ikiendelea kuboresha huduma zake huku ikijikita katika matibabu ya teknolojia ya hali ya juu






No comments:
Post a Comment