MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AWASILISHA MAJIBU KUHUSU MUSWADA WA SHERIA NA.2 WA 2026 - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, August 18, 2026

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AWASILISHA MAJIBU KUHUSU MUSWADA WA SHERIA NA.2 WA 2026


Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imewasilisha majibu ya Serikali kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge Utawala, Katiba na Sheria kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.2) wa Mwaka 2026 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments ) (No.2) Bill, 2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria tarehe 18 Agosti, 2026 Bungeni Jijini, Dodoma.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari ameliongoza jopo la Wataalamu wa Sheria katika kuwasilisha majibu ya Serikali kuhusiana na Muswada huo.

Mwandishi Mkuu wa Sheria, Bw. Onorius Njole amezitaja Sheria zinazokusudiwa kufanyiwa marekebisho ni pamoja na
Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori Sura ya 283, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287, Sheria ya Utathimini na Usajili wa Wathamini, Sura ya 138, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Sura ya 288, Sheria ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi, Sura ya 116.o

No comments:

Post a Comment