TASAC YATOA ELIMU YA UTUNZAJI MAZINGIRA DODOMA - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Monday, June 2, 2025

TASAC YATOA ELIMU YA UTUNZAJI MAZINGIRA DODOMA



Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania TASAC, leo tarehe 02 Juni, 2025 limetoa elimu ya utunzaji wa mazingira majini kwa wadau waliotembelea banda lao jijini Dodoma.

TASAC imetoa elimu hiyo kwa wadau na wananchi wa Dodoma katika Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani 2025 yanayofanyika kuanzia tarehe 01 - 05 Juni, 2025 jijini humo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wataalamu wa TASAC wameeleza wananchi namna wanavyotekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na jukumu la kusimamia na kudhibiti Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa Mazingira pamoja na kupambana na umwagikaji wa mafuta majini.

Baadhi ya wadau waliotembelea banda hilo ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Ladislaus Chang’a ambapo amepongeza juhudi za TASAC katika kutumia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na TMA.

TASAC ni moja ya taasisi za umma zinazoshiriki maadhimisho hayo yenye kauli mbiu: “Mazingira Yetu na Tanzania Ijayo Tuwajibike Sasa, Dhibiti Matumizi ya Plastiki”. Kilele cha maadhimisho hayo ni tarehe 05 Juni 2025.




No comments:

Post a Comment