WAZIRI WA MADINI ATOA TUZO KWA POLISI DODOMA. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, June 11, 2025

WAZIRI WA MADINI ATOA TUZO KWA POLISI DODOMA.



Chama Cha Bodaboda na Bajaji Mkoa wa Dodoma (UMAPIDO), kimepongeza jitihada za Jeshi la Polisi Mkoani hapo kwa kuwezesha uzinduzi wa Ofisi ya Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) cha umoja huo.

Akizungumza katika uzundunzi huo Juni 11,2025 kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwamdamizi wa Polisi George Katabazi amesema Jeshi la Polisi la mbali na kuchangia fedha za ukamilishwaji wa chama hicho pia linatambua mchango wa maafisa hao katika kuzuia na kutanzua uhalifu.

Aidha katabazi amewataka wanachama hao kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi katika nyanja mbalimbali hususani kukemea uhalifu kuelimisha umma juu ya matumizi sahihi ya barabara pamoja na kuheshimu sheria za usalama barabarani.

Katibu wa Chama Cha Boda boda na bajaji Mkoa wa Dodoma Yusufu Mwamonje amesema Jeshi la Polisi limekuwa na mahusiano mazuri na chama hicho kwa kuinua uchumi wa chama, upatikanaji wa leseni kwa madereva hao pamoja na kushiriki katika mabonanza ya michezo
yaliyo kuwa yakiandaliwa na jeshi la polisi chini ya Rpc Katabazi ikiwemo
ligi mbalimbali za mpira wa miguu Polisi Family Day, pamoja na kuandaa mikutano ya kuhamasisha vikundi vya ulinzi shirikishi.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo Waziri wa Madini Mhe, Athony Mavunde amepongeza chama hicho kwa kufanya mageuzi yatakayo changia maendeleo kwa kila mwana chama

Vilevile, Mavunde ameeleza umuhimu wa kushirikiana na Jeshi la Polisi katika sekta hiyo ya usafirishaji pamoja na kutoa tuzo ya heshima kwa kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma (SACP), Katabazi kwa kuwaongoza askari kutoa huduma bora kwa wananchi wa Dodoma na kuimarisha ulinzi na usalama.




No comments:

Post a Comment