
Picha mbalimbali za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mkutano wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo Septemba 13, 2025. Dkt. Samia anawania nafasi hiyo mara baada ya kuwa na mafanikio makubwa kwenye utekelezaji wa ahadi na Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa 2020 katika kipindi cha miaka minne aliyoongoza Tanzania, akifanikiwa kukamilisha na kuendeleza vyema miradi mbalimbali ya kimkakati pamoja na utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii kwenye sekta za afya, maji, elimu, miundombinu na huduma nyinginezo.








No comments:
Post a Comment