
Na Mwandishi Wetu, Geita
Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imekuwa kivutio pekee kwa taasisi za Serikali zinazoshiriki katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita.
Ushiriki wa REA katika maonesho hayo umevutia wananchi wengi kutembelea banda la Wakala ambapo wataalam kutoka REA wanaendelea kutoa elimu ya miradi mbalimbali ya REA inayotekelezwa hapa nchini kwa mafanikio pamoja kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kusambaza na kuuza majiko banifu kwa bei ya ruzuku na majiko ya gesi.


No comments:
Post a Comment