WAZIRI KIKWETE ASEMA SERIKALI ITAENDELEA KUWAHUDUMIA NA KUWAENZI VIONGOZI WA KITAIFA WASTAAFU KWA MCHANGO WAO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA TAIFA - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, March 17, 2026

WAZIRI KIKWETE ASEMA SERIKALI ITAENDELEA KUWAHUDUMIA NA KUWAENZI VIONGOZI WA KITAIFA WASTAAFU KWA MCHANGO WAO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA TAIFA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (hayupo pichani)
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kushoto) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Wananchi mbalimbali wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Askofu wa Jimbo Katoliki Rulenge Ngara, Mhashamu Severine Niwemugizi akiongoza Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.

Na Veronica Mwafisi-Chato


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Serikali itaendelea kuwahudumia na kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa kiwango stahiki kwa mujibu wa sheria na kwa kuzingatia maelekezo ya mara kwa mara yatakayotolewa na Mamlaka.
Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo tarehe 17 Machi 2026 kwenye kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita.

Amesema, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ndiyo yenye dhamana na Matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa Mujibu wa Hati Idhini ambayo Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aligawa majukumu kwa Mawaziri na suala hili la kumbukizi ni mojawapo ya utekelezaji wa Sheria ya Mafao ya Hitimisho la Kazi kwa Viongozi wa Kisiasa Sura 225 jambo ambalo hata Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, aliwahi kulitolea maelekezo.

Kwa msingi huo, tunatoa uhakika wa uendelevu wa huduma bora kwa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu na Wajane wa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, amesisitiza Mhe. Kikwete.

Aidha, ameongeza kuwa Rais wa Awamu ya Tano alielekeza kuwa suala la kumbukizi linatakiwa kufanyika kwa umakini na ubora wa hali ya juu ili kuwafanya viongozi waliostaafu na wanaojiandaa kustaafu kuwa na ari ya kufanya kazi kubwa ya kulijenga Taifa wakiwa kazini kutokana na kupata uhakika wa uendelevu wa mustabali wa maisha yao na kuweka misingi bora ya kukabidhi kijiti cha uongozi wa nchi yetu.

Mhe. Kikwete amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ruhusa na maelekezo mbalimbali kuhusu kufanyika kwa kumbukizi hiyo. 

“Nikiwa ndiye Waziri mwenye dhamana na matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu naomba nikushukuru wewe binafsi kwa kutoa fedha za kufanikisha shughuli hii sambamba na kutusimamia katika kufanikisha jambo hili muhimu kwa Ofisi yetu, Serikali kwa ujumla na Familia ya Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo hapa inaongozwa Mama Janeth, Mjane wa Hayati Dkt. John P. J. Magufuli, ameongeza.

No comments:

Post a Comment